Millionaire  Ads

Monday, August 25, 2014

TIMU YA VETERAN SINGIDA YA ENDELEA KUJINOA.

Tags

Mojawapo ya timu ambazo zinafanya mazoezi kwa juhudi na kwa ratiba maalumu kwa mkoa wa Singida ni timu ya  Veteran Singida Timu ambayo imedumu kwa muda mrefu sasa tangu kuanzishwa kwake.
Timu hii inaundwa na Waamuzi, Makocha na Wachezaji waliostaafu soka kwa miaka kadha iliyopita, kwa hivyo timu hii imesheheni kila aina ya watu ambao wanaujuzi katika soka  kwani  mchezaji asipokuwa alikuwa Muamzi basi atakuwa alikuwa kocha na kama hakuwa kocha basi atakuwa alikuwa mchezaji hivyo Veteran hawa wamekuwa  mchango mkubwa  katika maendeleo ya michezo hasa mpira wa miguu.
Timu hii pamoja na malengo hayo mazuri  bado wadau walikuwa wanashauri kuwa itakuwa vema endapo itatumika kama Timu ya mafunzo  kwa wadau wa mpira wa miguu kwakuwa  kuna uwezekano mkubwa sana timu nyimgine zikawa zinajifunza kupitia timu hiyo kwa mfano.
  • Veterani ambao ni makocha wanaweza kuwafundisha wachezaji wengine toka timu nyingi namna nzuri ya kucheza mpira kwani asilimia kubwa za maveterani hawa walifanya vizuri enzi zao  wakiwa wanacheza, wanafundisha au wanachezesha mpira.
  • lakini pia maveterani ambao wamekuwa waamuzi wa muda mrefu wanaweza wakasaidi timu nyingine namna ya kutafsili sheria hali itakayo saidia timunyingine kucheza mchezo mzuri usiokuwa na makosa mengi  na ya mara kwa mara.
  • Upande wa wachezaji  wa timu hii wangesaidi kushauri timu nyingine maswala mazima ya nidhamu, Uzalendo, juhudi na ujasisili wa kutetea timu yao pindi wanapo kuwa mchezoni.
Mimi nafikiri hii itakuwa namna nzuri ya kuboresha timu zetu iliziweze kufanya vizuri katika michezo yake tofauti na sasa ambavyo timu hizi zimekuwa zikisusua sana katika mashindano
Ninashauri pia veterans wote kuwa karibu sana na timu hizi ambazo zinaibukia na kukosa mwelekeo baadaye.

 Timu ya veterani ikiwa katika mazoezi siku ya Jumamosi
 Mchezaji wa veterani akionesha ufundi wake katika kucheza  Soka
 Wachezaji wakijaribu kutumia mbinu tofauti tofauti katika kupiga na kupokea pasi .
 Timu ya veterani ikiwa katika mazoezi siku ya Jumamosi
 Timu ya veterani ikiwa katika mazoezi siku ya Jumamosi
Vijana hawa wazamani wakioneshana ufundi katika kupokea na kuumiliki mpira  sawia 

3 comments

KWELI TIMU ZETU SINGIDA ZIPO VIZURI SANA SEMA VIWANJA NDO TATIZO CHEKI VUMBI HILO NI SHIDAAAAA!!!

HAPANA CHEZEA.

hii nayo ni changamoto pia maana kuna kundi jingine halioni umuhimu wa viwanja hivi ndo maana hata uwanja wa namfua haukamiliki.

Changia mawazo yako hapa, Kuwa huru kuandika chochote kwa manufaa ya jamii
EmoticonEmoticon