Millionaire  Ads

Thursday, August 7, 2014

MUNGHANGA FOOTBALL ACADEMY ZA KWAANA VIKALI NA IBUN BUZ FOOTBALL CLUB UWANJA WA NAMFUA MJINI SINGIDA

lilikuwa ni pamabano la kuvutia baina ya timu mbili zilizo cheza jana jioni Uwanja wa mkoa wa Namfua. pambano hili lilihusisha timu mbili toka mjini singida ambazo ni Mughanga football Academy na Ibun buz. Pambano hili ni moja ya maandalizi  ya kujiandaa na Ligi ya Mkoa inayo tarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu 2014.Ligi hiyo itakuwa na dhumuni la kuweza kupata timu itakayo utetea mkoa wa Singida katika medali ya Soka dhidi ya mikoa mingine. Timu hizi zilimaliza mchezo ambapo Ibun bazi iliibuka na na ushindi wa goli moja kwa bila (Sifuri) dhidi ya Mughanga.
Nidhahili kwamba singida haija weza kupata timu mwakilishi wa Mkoa katika mashindano makubwa ya daraja la kwanza na ligi kuu kwa mda mrefu sasa. kuna maswali mengi pia ambayo bado hayaja patiwa majibu aidha kwa kukosekana majibu hayo au kwa kuwepo majibu yasiyo kuwa na mashiko vichwani mwa wadau.
Maswali haya nikama:-
  1. Kiko wapi kizazi kilicho utetea mkoa wa Singida ndani ya Singida United na kindai Shooting?
  2. Uko wapi uongozi ulio pigana kufa na kupona  miaka ya ushindi wa Taifa cup?
  3. Wako wapi wadau walio pandisha timu miaka ya Samaria ya Itigi?
  4. Uko wapi mpira uliochezwa enzi za Mto Fc?
lakini pia swali jingine linalo kuna vichwa wadau  ndani na nje ya Mkoa wa Signida ni lile la  uwepo wa viwanja vizuri kabisa  vyenye magoli ya kisasa kwa kila kijji kwa mkoa wote wa singida, Hali ambayo nifursa ya pekee kwa mkoa huu. Ipo haja sasa ya kupanga mikakati endelevu isiyo tanguliwa na maslahi binafsi itakayo tutoa hapa tulipo kutupeleka mahali pengine pazuri zaidi.
 Nafikiri sasa umefika wakati wa viongozi wa mpira wa miguu Mkao kushirikiana na serikali ya mkoa kuwekeza mawazo, Muda na Mali katika michezo kwani Singida ni moja ya mikoa inayo weza kunufaika sana na Ajira kupitia michezo kuliko mikoa mingine  ikutokana na fursa zilizopo, asili na historia ya mkoa, hali ya hewa pamoja na uwepo wa wadau waliowekeza katika eneo la michezo.
kwa mfano Mradi wa michezo wa TTU-Education Through Sports Singida, Miradi mingi ya michezo inayo fadhiliwa na Mh.Mbunge Bwana  Mohamed Dewji (Mo cup).

Wachezaji wa Mughanga Football academy Ibun Buz Footbal Club  wanasaliamiana tayari kwa kuanza mchezo.

Mwl. Abdallah Mwinyimkuu katikati ndiye muamzi wa mchezo huu akisaidiwa na Muamzi wa kwanza kushoto kwake  Fredrick Ndahani  na pia kulia kwake ni mwamzi msaidizi Pili Deusi


vijana  wako tayari kwa kuanza mchezo timu zote mbili



waamuzi wakisalimiana na makapteni wa timu zote mbili

Waamuzi wakitambaulishana na makepteni wa timu na kuelekezana utaratibu wa mchezo.

Wednesday, August 6, 2014

WAAMUZI WA MPIRA WA MIGUU WAWAKIVUTIO KWA WADAU WA SOKA MKOANI SINGIDA

Kutokana na mikakati inayo fanywa na chama cha waamuzi wa mpira wa miguu mkoani Singida (FRAT) kumekuwa na utaratibu kabambe ulio ratibiwa na  Waamuzi wa ligi Kuu na FIFA wanaotoka Mkoa wa Singida. Chama hiki kimekuwa mfano wa kuigwa mkoani Singida. ubora huu umetokana na waamuzi kuwa na vipindi vya kufanya mazoezi kwa pamoja na pia kukaa na kupitia sheria Kumi na saba za soka kwa pamoja pia hali imepelekea chama hiki kiwe na mshikamano mzuri sana.
Wadau wa Mpira pia wameenda mbali kwa kupongeza  uongozi wa chama cha waamuzi wa soka  na Chama cha Mpira Mkoa  wa Singida.
Ikumbukwe pia chama hiki mwanzoni mwa mwaka kilipatwa pigo la kuondokewa na Mwanyekiti wachama  hayati Bw.Josephati Magazi ambaye pia alikuwa mkufunzi mkuu wa Wawaamuzi wa mpira wa miguu kwa mkoa wa Singida na  Mechi Kamishina wa ligi kuu kwa zaidi ya miaka kumi na mbili, hata hivyo kutokana na miongozo yake mizuri  waamuzi wameendelea kumuenzi kwa kushikamana na kuendelea kuwa wamoja na wenye nia ya kuhakikisha wanakuwa wadau halali wa mpira wa miguuua kwa kufuata miongozo na kanuni zinazo simamia chama.
kwa hili hongera chama cha Waamuzi mkoa wa singida na hongera waamuzi wa ligi kuu na FIFA kwa kuwa msitari wa mbele kuwaongoza waamuzi wenzenu na kuwa saidia kimazoezi.

Waamuzi wa mpira wamiguu Mkoa wa Singida wakiwa katika majadiano baada ya mazoezi  siku ya Juma mosi katika uwanja wa mkoa wa Namfua Singida.

 Waamuzi wa mpira wa miguu wakiwa katika  zoezi la kuunyosha mwili baada ya mazoezi
Picha  juu ni Darasa la waamuzi wa mpira wa miguu Mkoa wa Singida wakiwa katika mafunzo ya sheria kumi na saba za soka chini ya wa kiongozwa na Mwl. Arnold Bugado ambaye pia ni Mwamzi wa daraja la kwanza na anachezesha michezo ya Ligi kuu Tanzania bara.