Home
All posts
Friday, August 8, 2014
MRADI USIO WA KISERIKALI WA TTU-EDUCATION THROUGH SPORTS WAENDESHA TAMASHA LA MICHEZO KWA WANAFUNZI WALEMAVU.
Wanafunzi zaidi ya miamoja viziwi kutoka Shule ya Msingi ya Tumaini iliyopo Manispaa ya Singida wameshiriki katika tamasha la michezo lililoendeshwa na Mradi usio wakiserikali wa TTU-Education Through Sports Mradi unao husika na maendeleo ya michezo Mkoa wa Singida.
Michezo iliyo husishwa katika tamasha hilo ni Riadha Wavulana na Wasichana ambapo walikimbia na kutupa, Mpira wa Miguu Wavulana na Wasichina na Mpira wa Wawavu ambapo nao walicheza wavulana na wasichana.
katika hali isiyo ya kawaida wanafunzi hawa walifurahi sana hali iliyowapelekea hata kutaka kuendelea na mchezo licha ya muda wakucheza kuwa umeisha.
Mwalinu Mkuu wa shule hii Bw. Francis alikili kuwa wanafunzi wamefurahi sana hatawakakataa kwenda kula pindi muda wakula ulipowadia.
Akizungumza na wanafunzi wakiwa na Walimu wao, Meneja wa Mradi wa TTU-Education Through Sports Bw. Arnold Bugado alisema kuwa Mradi umekuwa ikijitahidi kuishawishi jamii pamoja na wadau ilikuona watoto walemavu wanahusishwa katika michezo kikamilifu.pia alisema sehemu nyingi utakapokuta michezo ikifanyika ni mara chache sana kukuta ikiwashirikisha walemavu, hivyo basi ni dhahiri kuwa kundi hili limesahaulika sana katika jamii yetu.
Meneja aliendelea kuwasihi walimu kuwa wavumilifu na kuendelea na moyo ambao wamekuwa nao kwani muda mwingi wamekuwa wakiutumia kuwalea watoto walemavu na kuwafundisha.
Shule ya msingi Tumaini ni shule ambayo imejikita na ufundishaji wa Wanafunzi Viziwi (wasiosikia wala kuaongea) lakini pia shule hii imekuwa ikikabiliwa na changamoto nyingi kama vile Msukumo mdogo kutoka kwa jamii, kutokuwapo na Mabweni ya wanafunzi na uchache wa vifaa vyakujifunzia na kufundishia vilivyo maalumu kwa wanafunzi wenye ulemavu huo.
Mradi wa TTU- Education Through Sports ulitoa zawadi kwa wanafunzi hao ikiwa ni pamoja na Jezi za michezo anuai, viatu vya mpira na vya mazoezi, Mifuko midogo ya kuwekea vifaa vya shule na zawadi nyingine nyingi.
Tunawashukuru Uongozi wa Mradi huo kwa kujitolea kwao.
Karibu utuambie sehemu uliyoko kundi hili lina nafasi gani katika michezo.
Michezo iliyo husishwa katika tamasha hilo ni Riadha Wavulana na Wasichana ambapo walikimbia na kutupa, Mpira wa Miguu Wavulana na Wasichina na Mpira wa Wawavu ambapo nao walicheza wavulana na wasichana.
katika hali isiyo ya kawaida wanafunzi hawa walifurahi sana hali iliyowapelekea hata kutaka kuendelea na mchezo licha ya muda wakucheza kuwa umeisha.
Mwalinu Mkuu wa shule hii Bw. Francis alikili kuwa wanafunzi wamefurahi sana hatawakakataa kwenda kula pindi muda wakula ulipowadia.
Akizungumza na wanafunzi wakiwa na Walimu wao, Meneja wa Mradi wa TTU-Education Through Sports Bw. Arnold Bugado alisema kuwa Mradi umekuwa ikijitahidi kuishawishi jamii pamoja na wadau ilikuona watoto walemavu wanahusishwa katika michezo kikamilifu.pia alisema sehemu nyingi utakapokuta michezo ikifanyika ni mara chache sana kukuta ikiwashirikisha walemavu, hivyo basi ni dhahiri kuwa kundi hili limesahaulika sana katika jamii yetu.
Meneja aliendelea kuwasihi walimu kuwa wavumilifu na kuendelea na moyo ambao wamekuwa nao kwani muda mwingi wamekuwa wakiutumia kuwalea watoto walemavu na kuwafundisha.
Shule ya msingi Tumaini ni shule ambayo imejikita na ufundishaji wa Wanafunzi Viziwi (wasiosikia wala kuaongea) lakini pia shule hii imekuwa ikikabiliwa na changamoto nyingi kama vile Msukumo mdogo kutoka kwa jamii, kutokuwapo na Mabweni ya wanafunzi na uchache wa vifaa vyakujifunzia na kufundishia vilivyo maalumu kwa wanafunzi wenye ulemavu huo.
Mradi wa TTU- Education Through Sports ulitoa zawadi kwa wanafunzi hao ikiwa ni pamoja na Jezi za michezo anuai, viatu vya mpira na vya mazoezi, Mifuko midogo ya kuwekea vifaa vya shule na zawadi nyingine nyingi.
Tunawashukuru Uongozi wa Mradi huo kwa kujitolea kwao.
Karibu utuambie sehemu uliyoko kundi hili lina nafasi gani katika michezo.
Subscribe to:
Posts (Atom)