Millionaire  Ads

Friday, August 8, 2014

MRADI USIO WA KISERIKALI WA TTU-EDUCATION THROUGH SPORTS WAENDESHA TAMASHA LA MICHEZO KWA WANAFUNZI WALEMAVU.

Wanafunzi zaidi ya miamoja  viziwi kutoka Shule ya Msingi ya Tumaini  iliyopo Manispaa ya Singida wameshiriki katika tamasha la michezo lililoendeshwa na Mradi usio wakiserikali wa TTU-Education Through Sports  Mradi unao husika  na maendeleo ya michezo Mkoa wa Singida.
Michezo iliyo husishwa katika tamasha hilo ni Riadha  Wavulana na Wasichana ambapo walikimbia na kutupa, Mpira wa Miguu Wavulana na Wasichina na Mpira wa Wawavu ambapo nao walicheza   wavulana na wasichana.
katika hali isiyo ya kawaida wanafunzi hawa walifurahi sana hali iliyowapelekea hata kutaka kuendelea na mchezo licha ya muda wakucheza kuwa umeisha.
 Mwalinu Mkuu wa shule hii Bw. Francis alikili kuwa wanafunzi wamefurahi sana hatawakakataa kwenda kula pindi muda wakula ulipowadia.
Akizungumza na wanafunzi wakiwa na Walimu wao, Meneja wa Mradi  wa TTU-Education Through Sports Bw. Arnold Bugado alisema kuwa Mradi umekuwa ikijitahidi kuishawishi jamii pamoja na wadau ilikuona watoto walemavu wanahusishwa katika michezo kikamilifu.pia alisema sehemu nyingi utakapokuta michezo ikifanyika  ni mara chache sana kukuta ikiwashirikisha walemavu, hivyo basi ni dhahiri kuwa kundi hili limesahaulika sana katika jamii yetu.
Meneja aliendelea kuwasihi walimu kuwa wavumilifu  na kuendelea na moyo ambao wamekuwa nao kwani  muda mwingi wamekuwa wakiutumia kuwalea watoto walemavu na kuwafundisha.
Shule ya msingi Tumaini  ni shule ambayo imejikita na ufundishaji wa Wanafunzi Viziwi (wasiosikia wala kuaongea) lakini pia shule hii imekuwa ikikabiliwa na changamoto nyingi kama vile Msukumo mdogo kutoka kwa jamii, kutokuwapo na Mabweni ya wanafunzi na uchache wa vifaa vyakujifunzia na kufundishia  vilivyo maalumu kwa wanafunzi wenye ulemavu huo.
Mradi wa TTU- Education Through Sports  ulitoa zawadi kwa wanafunzi hao ikiwa ni pamoja na Jezi za michezo anuai, viatu vya mpira  na vya mazoezi, Mifuko midogo ya kuwekea vifaa vya shule na zawadi nyingine nyingi.
 Tunawashukuru Uongozi wa Mradi huo kwa kujitolea kwao.





Karibu utuambie  sehemu uliyoko kundi hili lina nafasi gani katika michezo.





Thursday, August 7, 2014

MUNGHANGA FOOTBALL ACADEMY ZA KWAANA VIKALI NA IBUN BUZ FOOTBALL CLUB UWANJA WA NAMFUA MJINI SINGIDA

lilikuwa ni pamabano la kuvutia baina ya timu mbili zilizo cheza jana jioni Uwanja wa mkoa wa Namfua. pambano hili lilihusisha timu mbili toka mjini singida ambazo ni Mughanga football Academy na Ibun buz. Pambano hili ni moja ya maandalizi  ya kujiandaa na Ligi ya Mkoa inayo tarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu 2014.Ligi hiyo itakuwa na dhumuni la kuweza kupata timu itakayo utetea mkoa wa Singida katika medali ya Soka dhidi ya mikoa mingine. Timu hizi zilimaliza mchezo ambapo Ibun bazi iliibuka na na ushindi wa goli moja kwa bila (Sifuri) dhidi ya Mughanga.
Nidhahili kwamba singida haija weza kupata timu mwakilishi wa Mkoa katika mashindano makubwa ya daraja la kwanza na ligi kuu kwa mda mrefu sasa. kuna maswali mengi pia ambayo bado hayaja patiwa majibu aidha kwa kukosekana majibu hayo au kwa kuwepo majibu yasiyo kuwa na mashiko vichwani mwa wadau.
Maswali haya nikama:-
  1. Kiko wapi kizazi kilicho utetea mkoa wa Singida ndani ya Singida United na kindai Shooting?
  2. Uko wapi uongozi ulio pigana kufa na kupona  miaka ya ushindi wa Taifa cup?
  3. Wako wapi wadau walio pandisha timu miaka ya Samaria ya Itigi?
  4. Uko wapi mpira uliochezwa enzi za Mto Fc?
lakini pia swali jingine linalo kuna vichwa wadau  ndani na nje ya Mkoa wa Signida ni lile la  uwepo wa viwanja vizuri kabisa  vyenye magoli ya kisasa kwa kila kijji kwa mkoa wote wa singida, Hali ambayo nifursa ya pekee kwa mkoa huu. Ipo haja sasa ya kupanga mikakati endelevu isiyo tanguliwa na maslahi binafsi itakayo tutoa hapa tulipo kutupeleka mahali pengine pazuri zaidi.
 Nafikiri sasa umefika wakati wa viongozi wa mpira wa miguu Mkao kushirikiana na serikali ya mkoa kuwekeza mawazo, Muda na Mali katika michezo kwani Singida ni moja ya mikoa inayo weza kunufaika sana na Ajira kupitia michezo kuliko mikoa mingine  ikutokana na fursa zilizopo, asili na historia ya mkoa, hali ya hewa pamoja na uwepo wa wadau waliowekeza katika eneo la michezo.
kwa mfano Mradi wa michezo wa TTU-Education Through Sports Singida, Miradi mingi ya michezo inayo fadhiliwa na Mh.Mbunge Bwana  Mohamed Dewji (Mo cup).

Wachezaji wa Mughanga Football academy Ibun Buz Footbal Club  wanasaliamiana tayari kwa kuanza mchezo.

Mwl. Abdallah Mwinyimkuu katikati ndiye muamzi wa mchezo huu akisaidiwa na Muamzi wa kwanza kushoto kwake  Fredrick Ndahani  na pia kulia kwake ni mwamzi msaidizi Pili Deusi


vijana  wako tayari kwa kuanza mchezo timu zote mbili



waamuzi wakisalimiana na makapteni wa timu zote mbili

Waamuzi wakitambaulishana na makepteni wa timu na kuelekezana utaratibu wa mchezo.